Advancing

For you

I drew a line for you,
A broken line,
All that you are,
Your skin,
Your bones,
Your blood,
Your strengths and weaknesses,
A true depiction of beauty.

Our dreams,
The talk,
The arguments,
The cries,
The smiles and laughter,
The broken promises,
All add up to even more,
Trust truth and redemption,
Strengthening the broken pieces.

Standard
Advancing

Little voices

I wish you saw,
You understood,
You realized,
Or even felt,
How you make me feel,
Being part of you.

Your presence,
Smile,
Talk,
Touch,
A look into your eyes,
Beauty allover,
Things that make me happy,
Longing for more.

Dreams of you,
Wishes,
Screams in my head,
A world that you have created,
Inside of me,
Pushing against the walls,
Waiting for the moment,
To take us higher,
Forever!

Standard
Advancing

Hitaji…

Matarajio ya ubora,
Hamu ya usasa baadaye,
Bidii na uchovu,
Jasho la ukakamavu,
Yote kwa maana ya kufaulu,
Mwishowe kuondoka bila,
Dunia tu wasafiri tu!

Kwa hali ya kuishi,
Wakati mwingine,
Huwa kuna haja,
Ya mja anayekupa muda,
Zaidi nafsi yake,
Na hamu ya kuelewa,
Kujua yote yaendeleayo,
Mvutano wa nafsi yako,
Kukuelewa na kushiriki nawe,
Katika mazungumzo yako ya kindani,
Bila ya kujali lolote,
Wala kukushtumu,
Ama kukudhania vitofauti.

Msukumo wa aina yake,
Labda tu kimawazo,
Hutuepusha na ukweli,
Kutuchochea na kutukosanisha,
Na wale tuwaenzio kimaisha,
Kwa kutupatia hamu zisizo,
Hamu ya vile tudhaniavyo,
Kuwa ni tofauti na hiki au kile,
Njaa ya kimawazo,
Tamaa iso’ na dawa.

Standard
Advancing

Hali yetu

Hivi ndivyo tulivyo. Undugu umetutoka. Hamna cha kaka wala dada. Tujuacho ni umimi na uwewe. Ingawa ni kweli kuwa kila mja alizaliwa pekee yake, mwanadamu ni kufaana. Nikune leo wayoni na kesho unapohitaji, nitakukuna mgongoni. Tuwache kuishi kana kwamba matatizo tul’o nayo hayatatutoka ikiwa hatutammaliza yule tumdhaniaye kuwa ni adui wetu.

Makabila ni mawili tu hapa tunapoishi. Tajiri na maskini. Au tuseme mtawala na mtawaliwa. Tunapowapatia watawala nguvu na mamlaka, wao hutugeuka na kutaka mamlaka na nguvu zaidi ili wabakie pale na kumkanyaga kabisa yule wanaomtawala ili asije kuropokwa au kukatizia starehe zao. Kuchovya mali ya umma na kulaghai ndio wajibu wao. Hata yule as’o na gari au mparapata anasukumwa kusaidia ujenzi wa barabara.

Standard